Jumatatu, 4 Julai 2016



KWANGU HUNA MWENZA



1. Moyo hausemezeki,   na akili iko pweke
Mwengine hanimiliki, yeye kipenzi peke
Milele simbanduki,      nataka mahaba yake
Tuwaache wenye chuki, penzi sitetereke.

2. Nianze wapi kukusifu,   angalau usifike
Umbile la Ashrafu,      sina budi nitamke
Ametukuka Latwifu,  kakupamba mja wake
Na kukupa maelfu,      ya vipaji vitumike.

3. Umepewa maelfu,      ya uzuri utumike
Kwenye yalo maarufu, yasifiwayo kwa mke
Kwako wewe nimekifu, kusudi nisisumbuke
Uninukishe harufu,        na wardi lichanuke

4. Toka juu hadi chini,       inapasa usifike
     Nywele ndefu na laini,   na macho yenye upeke
Tabasamu mdomoni,      uzuri wa umbo lake
         Ahsante na shukrani,      mevifanya wimbo wake.

         5. Uwe ni kama barafu,     mtima wangu shwarike
Na kwa moyo mkunjufu, pendo lako nifunike
Niipate tahafifu,           na maradhi yaponyeke
Nakupenda maradufu, sauti yangu sikike

Maoni 1 :

  1. kweli chawakama-suza mumeamua mwaka huu hongereni

    JibuFuta