Jumatatu, 4 Julai 2016


TUZIENZI MILA ZETU
 
1.      Bismilahi Azizi,           nataka kuelezeni
Nizidishie na pumzi,        niwaeleze wandani
Bila kuwa pingamizi,  nioneshe ya moyoni
Bustani tuenzi,             izidishe kushaini

2.      Nieleze waziwazi,       vijana wa visiwani
Utamaduni tuenzi,      na asili ya zamani
Vizazi tuviaidhi,          wasivamie mageni
Bustani ndio enzi,       kwetu sisi wezanguni

3.      Tujuwe mavazi yetu, mababu waloshaini
Hawakukubali katu,    wigi modo kusheheni
Kanzu mavazi yetu,    kwa nini hamutakani
Utamaduni ni wetu,    mzaha tuuwachie.

4.      Si kanga si mrekani,    hata lugha namba wani
Mwambao ndio makini, vilugha vi mitaani
Kizungu ni lugha gani,  nawauliza makwini
Utamaduni ni wetu,    mzaha tuuwacheni.

5.      Naacha kalamu yangu, nadhani nakuchosheni
Ikiwa wazimu wangu, mutanijadili ndani
Au nawakumbusheni,  muuachie ugeni
Mila zetu turudie,        tusivamie mjini.

Bishara Mohamed Ali-SUZA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni