UCHAWINI KUNA MAMBO
1.
Ukitaka ngia huko, wallahi
utashituka
Utakutia vituko,
vivyo navyo patashika
Utajutia kuwepo, na
huruma kukushika
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
2.
Vizuu wa uchawini, kiwaona
tashituka
Tadhani ni
hayawani, hali imebadilika
Si kichwa si
miguuni, sura zao kama paka
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
3.
Viongozi wa wachawi imeni
imewatoka
Yao kwa hustawi, vizuu
kupukutika
Ta siku moja haiwi,
mmoja akasikika
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
4. Uchawini ni hatari, ukatili
meongoka
Kuna watu majabari,
tena wasotikisika
Wamekuwa majeuri, kwa
kile wanachotaka
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
5.
Ajira ya uchawini, kama ya mkwe na kaka
Mavunoye huyaoni,
ni viboko na kuchoka
Utaona kisirani, na
akili kukuruka
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
6.
Ukichoka uchawini, kamwe usijeropoka
Watakuweka pembeni,
na njaa itakufika
Ubakie masikini ,
iwe huna pa kushika
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
7.
Siku ukiwa na ombi, ndipo hapo
utachoka
Waonekana cha
zombi, ulokosa pa kushika
Utakuwa cha
mbirimbi, kwa kisu utakatika
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
8.
Mwisho naliweka tojo kuonesha nimefika
Uchawini si porojo,
kila mtu akacheka
Utanywishwa ta
mkojo, watu kimya kukuweka
Uchawini kuna
mambo, si kama yalivyo huku
NA: SALEH ZAHRAN ABDULLA- CHAWAKAMA-SUZA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni