NA:
HAITHAM HASSAN OMAR
SALEH ZAHRAN ABDULLA
SALUM ABBASS
CHAWAKAMA-SUZA
MAKALA MUHIMU JUU YA ISTILAHI MBALI MBALI
ZINAZOTUMIKA KATIKA UFUNDISHAJI NA MASUALA YA KIELIMU NA UJIFUNZAJI KATIKA LUGHA YA KISWAHILI
Makala hii itakuwa na
sehemu mbili ambazo ni fasili mbalmbali za msamiati. Lakini kwa sehemu ya pili
itakuwa na MISAMIATI mbalimbali inayotumika katika ufundishai na ujIfunzaji
Kwa kuanzia na fasili ya
neno “MSAMIATI ni kama ifuatavyo
Kwa
mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004), Msamiati ni jumla ya maneno katika
Lugha.
Kwa
mujibu wa Kamusi Teule ya Kiswahili (2014), Msamiati ni maneno yote magumu na
rahisi ya Lugha yoyote inayotumika.
Katika
sehemu hii tunaonesha misamiati mbalimbali yanayotumika katika ufundishaji na
ujifunzaji. Misamiati hiyo ni kwa lugha ya Kiswahili.
Kwa
hivyo, misamiati ni maneno yanayotumika katika lugha fulani, mara nyingi hutumika
kumaanisha maneno mapya au maneno yasiyojuulikana na watu wengi. Msamiati
hutumika kufafanua maana ya maneno yanayopatikana katika muktadha mbali mbali.
Mfano msamiati wa skuli, maneno yanayotumika sana katika mazingira hayo
hayawezi kutumika kiasi kikubwa katika mazingira mengine kama hospitali.
Yafuatayo ni misamiati (50) ya Kiswahili inayotumika katika uwanja wa elimu na
ufundishaji:
1. Upimaji (Assessment): Ni mbinu inayotumika katika kujua mafanikio ya
ufundishaji na ujifunzaji unavyoendelea
darasani. Msamiati huu ni katika uga wa upimaji.
2. Jaribio (Test): Ni namna ya upimaji ama kwa njia ya maswali au vitendo ili
kupima kama mada iliyosomeshwa imefahamika au haikufahamika.
Msamiati huu ni katika uga wa upimaji.
3. Muhula (Term): Ni kipindi maalumu kwa ajili ya masomo ambacho tathmini ya
jumla ya maendeleo ya masomo yote hufanywa. Msamiati huu ni katika uga wa
upimaji.
4. Ripoti (Report): Ni taarifa maalum inayoandaliwa skuli kwa maendeleo ya
wanafunzi katika masomo yao. Msamiati huu ni katika uga wa upimaji.
5. Takwimu (Almanac): Ni taarifa za ukweli kuhusu mwanafunzi zinazoonesha
maendeleo yake ya kusoma na kujifunza katika kipindi maalum. Msamiati huu ni
katika uga wa upimaji.
6. Alama (Marks): Ni alama zinazotolewa na mwalimu kuonesha daraja au
kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi katika somo. Msamiati huu ni katika uga wa
upimaji.
7. Matokeo (Result): Ni takwimu ya kazi zilizofanywa na mwanafunzi kuonesha
namna ya mafanikio na udhaifu wa tendo la kujifunza na kufundisha. Msamiati huu
ni katika uga wa upimaji.
8. Dodoso (Questionnaire): Ni zana au mbinu inayotumiwa na mwalimu kupata
taarifa za kina (halisi na sahihi) katika tendo zima la ufundishaji na
ujifunzaji. Msamiati huu ni katika uga wa upimaji.
9. Chemsha
bongo (Quiz): Ni fumbo au mafumbo yenye
lengo la kuchokoza udadisi na wepesi wa wanafunzi kujibu au kujiweka tayari na
tendo la kujifunza. Msamiati huu ni katika uga wa upimaji.
10. Maendeleo (Progress): Ni tathmini ya mwenendo mzima wa mwanafunzi katika
tendo la kujifunza ama kusonga mbele au kurudi nyuma. Msamiati huu ni katika
uga wa upimaji.
11. Mahihisho (Corrections): Ni tendo linalotumika kumrekebisha au kumkosoa
mwanafunzi ili asiweze kurejea tena kosa hilo na kujua usahihi wake. Msamiati
huu ni katika uga wa tathmini.
12. Tathmini (Evaluation): Ni njia inayotumika kupata taarifa ni kwa kiasi gani
malengo ya ufundishaji yamefikiwa kukifuatiliwa na maamuzi muafaka. Msamiati
huu ni katika uga wa upimaji.
13. Uwasilishaji (presentation): Ni msamiati unaotumiwa na mwalimu katika hatua ya
kufundisha ili kutoa maarifa mapya au muendelezo wa somo katika tendo la
kujifunza. Msamiati huu ni katika uga wa kufundisha.
14. Viwango (Standard): Ni msamiati unaotumika kutoa maelezo kuhusiana na vipi
wanafunzi wanapaswa kufika katika sehemu fulani kwenye matokeo yao. Msamiati
huu ni katika uga wa mitaala.
15. Azimio la kazi
(scheme of work): Ni buku maalumu la mwalimu linalomuongoza kufundishia mada
zilizovunjwavunjwa kutoka katika muhtasari ili zisomesheke kiurahisi katika
wiki, mwezi au muhula. Msamiati huu ni katika uga wa Mitaala.
16. Andalio
la somo (lesson plan): Ni
buku maalumu la mwalimu linalomuongoza kufundishia mada zilizovunjwavunjwa
kutoka katika azimio la kazi ili zisomesheke kiurahisi katika kila kipindi. Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
17. Njia (Methodology): Ni mbinu inayotarajiwa kutumika katika kufanikisha
suala zima la upatikanaji wa elimu kwa namna inavyofaa kwa wanafunzi husika. Msamiati
huu ni katika uga wa mitaala.
18. Mwendo (Course): Msamiati huu unatumika katika kujumuisha mwenendo mzima
wa masomo ambayo wanafunzi wanategemea kujifunza katika kipindi kilichokusudiwa.
Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
19. Mafanikio (Achievement): Msamiati huu unatumika katika kuonesha ni kwa jinsi
gani wanafunzi wamefanikiwa. Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
20. Rejea (Reference): Msamiati huu hutumika katika kumsaidia mwalimu na
mwanafunzi kufanya kazi zao na hata katika kujifunza na kufundishia pia kuonesha uthibitisho wa
kazi mbali mbali mbali za kitaaluma. Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
21. Maudhui (Content): Msamiati huu hutumika katika kuonesha mtiririko mzima wa
somo kuanzia mwanzo wa somo hadi mwisho wa somo. Msamiati huu ni katika uga wa
mitaala.
22. Ujuzi (Competence): Msamiati huu pia hutumika katika kuonesha maarifa
aliyoyapata mwanafunzi kutokana na kile alichojifunza baada ya kumaliza
somo. Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
23. Marekebisho (Adjustment): Ni msamiati ambao unatumika kuwaeka sawa wanafunzi, walimu
na hata watu wa mitaala pale endapo patatokezea kasoro au patajitokeza tatizo
lolote katika kazi zao. Msamiati huu ni katika uga wa mitaala.
24. Kompyuta (Computer): Ni zana au kifaa kinachotumika kutafutia elimu,
kuandikia, kuchorea picha na michoro mengine mbali mbali katika tendo zima la
kufundisha na kujifunza. Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
25. Maktaba (Library): Ni sehemu ambayo hutumika kwa kujisomea vitabu,
majarida, magazeti nakadhalika kwa ajili ya kujiongezea maarifa na ujuzi katika
tendo zima la kufundisha na kujifunza. Msamiati huu ni katika uga wa zana za
kufundishia.
26. Mabango (Posters): Ni aina ya zana au kifaa cha kufundishia na kujifunzia
ambazo hutumika kuonesha picha na michoro ya vitu mbali mbali ambavyo si rahisi
kuvileta darasani wakati wa usomeshaji. Msamiati huu ni katika uga wa zana za
kufundishia.
27. Kamusi (Dictionary): Ni aina ya kitabu ambacho hutumika kujua maana,
tahajia, miundo na matamshi ya maneno mbali mbali katika lugha kwa ajili ya
kujiengezea taaluma na misamiati. Msamiati huu ni katika uga wa zana za
kufundishia.
28. Runinga (Television): Ni kifaa ambacho hutumika katika kupata maarifa
mapya kwa njia ya kuona picha na kusikia taarifa na matukio mbali mbali katika
tendo zima la kujifunza kwa kutumia njia za kisasa za sayansi na teknolojia. Msamiati
huu ni katika uga wa zana za kufundishia.
29. Maigizo (Role play): Ni aina ya mbinu za kufundishia ambayo hutumiwa na
mwalimu darasani ili kujenga ari na shauku za wanafunzi katika kulipenda somo ili
lengo lililokusudiwa lifikiwe. Msamiati huu ni katika uga wa mbinu za
kufundishia.
30. Mjumuisho (Inclusive): Ni ufundishaji unaojumuisha pamoja wanafunzi walemavu
na wasio walemavu, unaotumika skuli katika kuondoa ubaguzi na unyanyasaji ili
wanafunzi waweze kujifunza kwa kushirikiana na kusaidiana. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
31. Takriri (Repetition): Ni mbinu ya inayotumiwa wakati wa ufundishaji
inayowafanya wanafunzi kurudiarudia neno au sentensi kwa lengo la kutilia mkazo
na kujenga kumbukumbu ya kudumu. Msamiati huu ni katika uga wa mbinu za
kufundishia.
32. Ushirikishaji (Participartion): Ni njia ya ushirikishwaji wa wanafunzi katika
somo, unaotumika kuwafanya wanafunzi wote wawe na utayari wa kutenda na
kujaribu wakati wote wa tendo la
kufundisha na kujifunza. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
33. Mazingira/Muktadha (context): Ni mazingira halisi au yakubuni yanayotumiwa ili
kuwawezesha wanafunzi kujenga ufahamu wa mada kwa urahsi zaidi pamoja na
kumsaidia mwalimu kufahamika ipasavyo katika ufundishaji wake. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
34. Ubunifu (Creations): Ni uwezo wa kutenda mambo mbali mbali unatumiwa na
mwalimu na wanafunzi katika kuonesha ustadi na umahiri wao katika tendo zima la
kufundisha na kujifunza. Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
35. Wakufunzi (Trainers): Ni wataalamu walioteuliwa kwa lengo la kutoa mafunzo
ya aina mbali mbali kwa walimu (TRAINERS) ambayo yatatumika kuboresha uwezo wao
katika utendaji na kupelekea mabadiliko katika utendaji wao wa kazi. Msamiati
huu ni katika uga wa mafunzo.
36. Kinasa
sauti (Tape recorder): Ni aina ya kifaa
ambacho hutumika kuwapa wanafunzi ujuzi wa kusikiliza maneno, hadithi na habari
mbali mbali kwa ajili ya kufanya uchunguzi na uchanganuzi wa kile
walichokisikia. Msamiati huu ni katika uga wa zana za kufundishia.
37. Mrejesho (Feedback): Ni taarifa au tathmini inayofanywa baada ya
utekelezaji wa jambo kufanyika kwa ajili ya uendelezaji au urekebishaji
kulingana na utendaji ulivyofanyika na
mara nyingi hufanywa mwishoni mwa utekelezwaji. Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
38. Motisha/kichocheo (Motivation): Ni hali au kitendo kinachofanywa na mwalimu wakati wa
kufundisha ili kuwafanya wanafunzi wapende na wavutike na somo kwa njia ya
kuwapongeza, kuwasifu, kuwapazawadi nakadhalika. Msamiati huu ni katika uga wa
ufundishaji.
39. Fikiri
(think): Ni msamiati anaotumia mwalimu anapotaka kuwambia wanafunzi waweze kutoa/
kuelezea dhana ya jambo fulani. Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
40. Sikiliza
(listen): Huu ni msamiati ambao hutumika pale mwalimu anapotaka asikilizwe
wakati anapofunisha ili aweze kueleweka au kufahamika. Msamiati huu ni katika
uga wa ufundishaji.
41. Jaribu
(try): Msamiati huu unatumika pale mwalimu anapomtaka mwanafunzi aweze kusema
au kuandika kitu/jambo kwa mujibu anavyoona au kuhisi kulingana na akili yake.
Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
42. Kufahamu
(to understand): Msamiati huu hutumika pale mwalimu pale mwalimu anapowauliza
wanafunzi kama wamefahamu juu ya lile alilofundisha au wanafunzi
wanapomuhakikishia mwalimu kama wameelewa juu ya lile walofundishwa. Msamiati
huu ni katika uga wa ufundishaji.
43. Uchambuzi
(analysis): Msamiati huu hutokezea pale wanafunzi endapo hawakufahamu katika
jambo fulani na kutaka ufafanuzi zaidi kutoka kwa mwalimu. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
44. Majadiliano
(discussion): Ni mbinu ambayo hutumika pale mwalimu anapowataka wanafunzi
waweze kujadili vipengele fulani katika mada anayoifundisha. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
45. Jibu
(answer): Ni mrejesho ambao hutumika pale mwalimu anapouliza suali na kutaka
kupatiwa jibu kuhusiana na lile alilouliza. Msamiati huu ni katika uga wa
ufundishaji.
46. Somo lililopita
(previous lesson): Msamiati huu hutumika pale mwalimu anapotaka aunganishe mawazo
ya wanafunzi kuhusu somo lake jipya kotokana na somo lililopita yaani
kuwakumbusha wanafunzi kutokana na somo lililopita ili waweze kuelewa kwa
urahisi somo jipya. Msamiati huu ni katika uga wa ufundishaji.
47. Soma
(read): Msamiati huu hutumika pale mwalimu anapotoa kipande cha habari na
kumtaka mwanafunzi aweze kusoma ili wenzake waweze kumsikiliza. Msamiati huu ni
katika uga wa ufundishaji.
48. Mtaala
(curriculum): Ni hati/nyaraka maalumu inayotumika kuorodhesha yale yote
yaliyopangwa kusomeshwa skuli yakiwa rasmi au sio rasmi. Msamiati huu ni katika
uga wa Mitaala.
49. Muhtasari
(syllabus): Ni kifaa cha mtaala kinachotumika kuorodhesha mada zote zinazopaswa
kufundishwa katika kila somo. Msamiati huu ni katika uga wa Mitaala.
50. Kujisahihisha
(self criticism): Ni msamiati unaotumiwa na mwalimu katika kumfanya mwanafunzi
aweze kujirekebisha mwenyewe na kutoa maoni yake katika somo kama limefahamika
au halikufahamika na hatua atakazozichukua kama mwanafunzi hajaweza
kujirekabisha. Msamiati huu ni katika uga wa Mitaala.
Misamiati
iliyotajwa hapo juu na ambayo hayakuainishwa katika uwanja wa Elimu na
ufundishaji, kiujumla misamiati hiyo ni muhimu sana katika tendo zima la
ufundishaji na ujifunzaji ambalo huwapelekea wadau wa elimu kama vile wakuza
mitaala, watafiti, walimu na mwanafunzi kupata usahihi wa taarifa zinazotolewa.
MAREJEO.
Bukagile, G. & Masebo, J. B. (2008). Kiswahili kwa shule za
sekondari: Kidato cha pili.
Nyambari Nyangwine publishers:
Dar-es-salaam, Tanzania.
Coombs, B. (1995). Succeful Teaching: Apractical Hand book. Heinemann Educational books LTD: USA.
Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Toleo la pili. (2004).Oxford University
Press: Kenya.
Katabaro, A . R. et al. (2003). Moduli ya somo la upimaji,
tathmini na utafiti. Taasisi ya Elimu Tanzania: Dar-es-salaam, Tanzania
Ndalu, A.E. et al. (2014). Kamusi
teule ya Kiswahili: kilele cha lugha. Toleo la kwanza. Printwell Industries
Ltd: Kenya.
Youssef K.Y. (1998). Dictionary of the Terms of Education:
Librairie du Liban Publishers: Beirut, Lebanon.